Apr 20, 2012

Nyimbo zenye mahubiri adimu...


Napenda saana ujumbe katika wimbo huu.Mpendwa hebu sikiliza kwa makini maneno ya wimbo huu then tafakari.Inasikitisha kwamba waimbaji hatuimbi tena nyimbo zenye kutoboa ukweli kama hizi,tunaimba zile nyimbo zenye maneno ambayo jamii inahitaji kusikia.
Ubarikiwe saana Mtumishi Munishi kwa kuimba bila kujali jamii itachukuliaje mahubiri yako,simamia katika kweli maana ndiyo itakayotuweka huru,

Hivi ni kwanini?

Mungu uketiye mahala pa juu sana pokea sifa na utukufu kwa ajili ya kunipa uzima katika siku ya leo tena.

Wapendwa kwanini mahubiri ya siku hizi yamelenga katika kutoa ujumbe wa kuhamasisha utoaji wa sadaka tu?Msisitizo unakua kwamba ili upate nyumba,gari,ajira na maisha mazuri ni utoe sadaka iliyo nono.Yaani ni panda mbegu iliyonona/sadaka ili upate mibaraka iliyonona.

Sikatai kila mtu anataka maisha mazuri lakini  maisha ya hapa duniani ni mafupi na tunapita tu,sasa kwa nini wasiweke mkazo katika mahubiri yatakayosaidia kutufikisha kule ambako tutakwenda kuishi maisha ya milele.?

Kila madhabahu inasisitiza watu kutoa tuuu,tena nakumbuka niliwahi kukutana na Mchungaji mmoja anatokea West Afrika akanambia kwamba yeye kanisa lake halipendi kuhubiri kwa kutumia vifungu vya biblia vinavyotishia watu kwamba wasipofuata maagizo ya Mungu watachomwa katika moto wa milele.Yeye kanisa lake linahubiri kuhusu jinsi ya kupata maisha mazuri tu hapa duniani.

Na yeye anaamini kwamba ukishaokoka kwa mara ya kwanza ukabatizwa na kumkiri Yesu kuwa bwana na mwokozi wako basi wewe tayari unakwenda mbinguni hata kama  untavuta sigara,au unazini ukiwa tayari umeshaokoka maana anadai kuokoka ni mara moja.

Nikamuuliza hata kama nimeokoka nikinywa pombe bila kutubu nitakwenda mbinguni?Nadhani swali hili lilimfanya adhani mim ni mnywaji wa pombe,na kwa vile alikua akihitaji nijiunge na kanisa lake akaniambia kwamba,kama nitakunywa pombe na nafsi yangu haitanisuta kuwa ninatenda dhambi basi nitakua sitendi dhambi na mbinguni nitakwenda bila kipingamizi.

Mchungaji huyu aliendelea kunieleza kwamba,mtu ukishaokoka dhambi zote utakazofanya baada ya kumpokea Yesu hutahitaji kuzitubu maana tayari wewe umeshaokoka na dhambi zako zote unazofanya zinafutwa automaticaly.

Nikamuuliza kwa kumwambia kwamba,unapooka unakua umemkana shetani na kazi zake zote sasa iweje mtu uwe mlokole na bado ufanye yanayotokana na kazi za shetani?Akanifafanulia kwamba,kuna stage za wokovu,akasema unapokua ndio umeokoka unakua wewe ni "baby born again) halafu unapokaa kwa muda ndani ya wokovu unakomaa na hivyo unakua "matured born again".Akasema a baby born again kwa sababu bado hajakomaa anaweza kutenda dhambi za hapa na pale ila akikomaa utendaji wake dhambi hupungua au kwisha kabisa lakini akasema a baby born again anayetenda dhambi na yule aliyekomaa asiyetenda au anayetenda kidogo kidogo wote watakwenda mbinguni kwa baba.

Niliagana na Mchungaji huyu kwa kumuomba akasome 1Yoh:3:8
"Atendaye dhambi ni wa ibilisi;kwa kuwa ibilisi hutenda dhambi tokea mwanzo."

Nimemaliza nilichotaka kusema,nakuacha na maneno haya Aliyoyasema Yesu kwa wanafunzi wake.
Mathayo Mtakatifu 24:4-5. "Yesu akajibu akawaambia,Angalieni mtu asiwadanganye.Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi."

2 Wakorintho 11:13-14 “Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo. Wala si ajabu,. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.” Kristo huyu wa uongo atakuja kuudanganya hata ulimwengu wote".

Apr 19, 2012

Ndugu yenu aliyepotea leo ameonekana



Heheee nacheka kwa aibu maana ni muda mrefu saana tokea nimefanya jambo hapa Ushuhuda Wangu.

Kwa kweli ni kwa sababu ya majukumu kuwa mengi.Hata hivyo siku zote mim nasema kwamba kuwa na mambo mengi ya kufanya  yenye kuboresha maisha yetu ni baraka na neema.

Unapokua busy sana kiasi cha kukosa hata muda wa kuwa na marafiki,au kukutana na ndugu na jamaa au pengine hata kushindwa kufanya mambo tunayopenda kufanya inaweza kutufanya tuchukie kuwa busy,nakujiona utafutaji wa maisha unatugeuza watumwa,lakini  siku nilipowafikiria wasomi ambao wanashinda majumbani bila kuwa na cha kufanya kwa kukosa ajira,au wanaotamani kupata mtaji japo waanzishe biashara yakuboresha maisha lakini hawana na hivyo kuishia kukaa majumbani bila cha kufanya au wagonjwa wanaolala majumbani na kushindwa kuhangaikia shughuli zao  roho ya ulalamishi ilinifa na tokea siku hiyo niliona kwamba mimi ni miongoni mwa wabarikiwa maana nimebarikiwa uwezo wa kuwa busy kuhangaikia maisha yangu bila kikwazo chochote.

Haya,tuachane na hayo,sasa umeshajua kwamba nilipotea sio kwamba nilikua na tatizo lolote wala sikuwa mgonjwa.

Leo naomba nikuulize mpendwa yeyote utakayebahatika kufika katika blog hii.

Je mpendwa wangu umeshawahi kuisikia sauti ya Mungu ikizungumza nawe?
Je unaamini kwamba Mungu anazungumza nasi kila mara?
Je unafahamu kwamba,shetani naye ana sauti yake inayojaribu kuzungumza nasi?(b)Utawezaje kuitofautisha sauti ya Mungu na sauti ya shetani?

Mim naisikia sauti ya Mungu,huwa ninaitii na vile vile zinapokuja sauti zingine zisizo toka kwa roho wa Mungu ninazifahamu maana roho wa Mungu aliyeko ndani yangu unisaidia kuzitambua haraka na ninazikemea.

Ni muhimu sana kufahamu jinsi ya kuifahamu na kuisikia sauti ya Mungu.

Kwa leo nitaishia hapa,ila nitafanya muendelezo wa topic hii muhimu ambapo na vifungu vya biblia vitatumika katika kueleweshana jambo hili.

Nawaacha katika mikono salama ya Mungu wetu,Mungu mwenye matendo makuu yasioelezeka na yenye kutisha kama nini.Tungekuje leo kama hangekua mweye huruma,mpole na mwenye kusamehe?

Mbarikiwe!

Oct 10, 2010

tuko safarini usijisahau

Bwana Yesu asifiwe.
inasikitisha kwamba baadhi yetu tunaishi hapa duniani as if tumeshafika mwisho wa safari yetu.
Napenda kuitumia jumapili ya leo kukukumbusha ya kwamba hapa duniani tunasafiri,hapa sio nyumbani kwetu,nyumbani kwetu ni kule alikotangulia Yesu kutuandalia makao.
Tafuta sehemu iliyotulia ukae peke yako uuchunguze moyo wako ili upate kujua ni kitu gani kinachoweza kusababisha usipate kibali cha kuingia kule katika mji wa ahadi ambako ndiko nyumbani kwetu kisha ujiepushe nacho kwani kule nyumbani kwetu hakuna kilicho kinyonge kitakachoingia.
MAY OUR LORD JESUS BE WITH ALL OFF YOU.
THANK YOU.

   msikilize Jím Reeves ushushie kaujumbe kangu.


Oct 8, 2010

Let His Love Empower You

  One study shows that children grow and flourish when they are approved, accepted and valued. But when a child is raised in an environment that is harsh and disapproving, when the child feels they aren't "good enough," it limits and affects self-esteem.

This study revealed that 59% of CEO's are firstborn children, which isn't surprising when you consider how most firstborn children are treated by their parents—everything that child does is so amazing! That first smile, that first word, that first step—each first is seen as the most magnificent event of the year. Even most grandparents marvel at and encourage every move of that firstborn child. The constant recognition builds confidence and security.

Did you know God sees you the same way? Regardless of whether you were the firstborn in your family or not, you are the apple of His eye. He will always treat you like His most valuable child. He applauds you every time you take a step of faith. He's always speaking encouraging words into your heart and saying, "You can rise higher. You can do all things. You can fulfill your destiny."

Let those words sink down into your heart today and allow them to build your confidence. When you receive God's love and encouragement, it will empower you to do more than you ever thought possible. With His love, you can wake up every day with an attitude of faith and expectancy. You don't have to live guilty or condemned; you don't have to feel like you don't measure up. You may have made some mistakes, but just like a parent helps their child when they are learning to walk, God will help you get right back up anytime you fall.

Do your part and instead of dwelling on all you've done wrong, receive His forgiveness and let it empower you to improve. Imagine Him smiling down on you right now. Embrace His love. Remember, you are His most prized possession, the apple of His eye!

MUNGU AWABARIKI

Oct 6, 2010

Christina Shusho - Bwana Umenichunguza



hii ni mojawapo ya nyimbo inayonibariki sana.
ubarikiwe sana christine.
naamini utakayetembelea site hii utabarikiwa na kibao hiki.
enjoy!
I get my strength from Christ. I WOULD BE ABSOLUTELY NOTHING AND COULD DO ABSOLUTELY NOTHING WITHOUT HIM. He is my rock, my fortress, my love for others, my faith, my shield, my courage, my heart, my soul….everything I am, I am because of him.

MBARIKIWE SANA